Thursday 17 July 2014

VAN GAAL ATUA MANCHESTER UNITED KWA NDEGE BINAFSI

VAN GAAL ATUA MANCHESTER  UNITED KWA NDEGE BINAFSI

Huku ushabiki na mbwembwe za kombe la dunia zikibaki kumbukumbu,ushabiki sasa unarudi vilabuni, wana- Manchester United, wanamwangalia kwa karibu kocha wao mpya Louis van Gaal, amekuja na miujiza gani?
Alipowasili kwenye uwanja wa mazoezi Carrington amesema hana jipya zaidi ya kujenga mshikamano zaidi miongoni mwa wachezaji.
'Ni lazima tuimbe wimbo huohuo ulioisaida timu ya Uholanzi ililowaezesha kukaribia ushindi wa kombe la dunia na kuibuka nafasi ya tatu kwa kuwafunga wenyeji Brazil' amesiitiza
Lakini ufafanuzi zaidi ataotoa katika mkutano na waandishi habari baadae leo.
Kikosi hicho cha Man United kikiwa na wachezaji wapya akina Herrera na Luke Shaw, waliopatikana kwa gharama ya zaidi ya £millioni 56m,wataelekea Marekani ijumaa kwa ziara na kucheza angalau mechi tano.KWA MSAADA WA BBC SWAHILI

No comments:

Post a Comment