Thursday 7 August 2014

MUME NA MKE WAISHI PAMOJA KWA MIAKA 62 NA WAFARIKI PAMOJA WAKIWA WAMESHIKANA MIKONO

Don na Maxime enzi za uhai wao huku wakiwa wamejawa na furaha


Don na Maxime wakiwa wameshikana mikono hata baada ya kufariki

Mume na mke walioishi pamoja kwa miaka 62 pamoja wameshangaza watu huko Marekani kwa kufariki siku moja huku wakiwa wameshikana mikono. Maxime ambaye ni mke na Don ambaye ni mume walipishana masaa manne tu ya vifo vyao. Maxime alikuwa mgongwa wa kansa wa siku nyingi huku mumewe alikuwa anasumbuliwa na maumivu ya nyonga. Siku yao ya mwisho ilikuwa pale walipotolewa hospitali na ndugu zao kurudishwa nyumbani ambapo Maxime alianza kufarikina mara tu baada ya Maxime kutolewa chumbani Don alifariki dunia.Kilichoshangaza zaidi ni kwamba walifariki dunia huku wakiwa wameshikana mikono.Haya ni mapenzi ya kweli ya kufa na kuzikana.

No comments:

Post a Comment